KUPOTEZA HAMU YA KULA KWA WATOTO


Kupoteza hamu ya kula kwa watoto: Sababu za kupoteza hamu ya kula na Jinsi ya kukinga tatizo hili.










·      Sababu za kupoteza hamu ya kula kwa watoto:
·      Jinsi ya kukinga kupoteza hamu ya kula kwa watoto:
·      Jinsi ya kuongeza hamu ya chakula kwa watoto.
·      Virutubisho vya kusisimua hamu ya kula.


Sababu za kupoteza hamu ya kula kwa watoto


1. kupungua kwa kasi ya ukuaji:
Mabadiliko ya ukuaji wa mtoto yanaweza kusababisha kupoteza hamu ya kula kwa mtoto. Kipindi cha mwaka wa kwanza, mtoto hukua kwa kasi sana, lakini baada ya hapo kasi ya ukuaji hupungua, na mtoto anaweza kuanza kula kidogo. Katika kipindi hiki kupungua kwa hamu ya kula kwa mtoto ni kawaida.

2. Maradhi:
Maradhi mara nyingi yanasababisha kwa kiasi kikubwa kupoteza hamu ya kula kwa watoto, kama mtoto anaumwa, tonsils, mafua, tumbo, kuharisha, kichwa, homa, na dalili nyinginezo, atakuwa anakula kidogo kuliko anavyopaswa kula, kwa bahati nzuri watoto wengi hamu ya kula hurejea wanapopata nafuu.

3. Msongo wa mawazo:
Inaweza kuonekana kuwa ni kitu kigeni/cha kushangaza lakini msongo wa mawazo ni hali ambayo inaweza kumpata mtoto pia, na ikamletea matatizo mengi ikiwemo na kupoteza hamu ya kula. Ukiona mtoto anapoteza hamu ya kula na anapata shida kulala, anaweza kuwa na msongo wa mawazo. Ili kumsaidia kuondokana na tatizo la kupeteza hamu ya kula kwa sababu ya msongo wa mawazo unapaswa kugundua sababu za msongo wa mawazo kwa watoto.
Baadhi ya sababu hizo ni:
·         Changamoto za familia kama msiba, kifo cha mnyama aliyepenwa na mtoto, kuzaliwa mtoto mwingine n.k
·         kuonewa
·         kushindwa kuendana na hali ya masomo.
·         Kuzuiliwa kufanya vitu anavyovipenda


6. Madawa:
Ikiwa mtoto amekuwa kwenye matumizi ya madawa mbalimbali hususani dawa za kuua backteria(antibaiotiki), hamu yake ya kula itapungua, kupoteza hamu ya kula kwa watoto hutokea kama maudhi madogo ya dawa mbalimbali.

7. Upungufu wa Damu:
Upungufu wa damu ni sababu pia ya mtoto kupoteza hamu ya kula, mtoto anayepitia changamoto hii, ataonekana mchovu sana, na mdhaifu sana, pia anakuwa msumbufu kwa wengine. Asipotibiwa tatizo hili atakuwa na ukuaji mbaya na atashindwa kufanya vizuri shuleni. Mpeleke mtoto apimwe damu kama utahisi ana upungufu wa damu.


8. Minyoo ya Tumboni:
Minyoo ya tumboni inaweza kumpotezea hamu ya kula mwanao. Minyoo huingia ndani ya mfumo wa chakula wa mtoto wako na kuishi humo kama tegemezi, wakisababisha kuvuja damu kwenye utumbo, kupoteza hamu ya kula, kuharisha damu n.k.

9. Kutopata Choo kubwa:
Kama utumbo wa mtoto hautakuwa katika mijongeo mizuri, mtoto hatapata choo, kupoteza hamu ya kula ni dalili halisi ya Kukosa Haja kubwa.


Kukosa hamu kwa mtoto kunaepukika kwa urahisi kwa kufuata mbinu zifuatazo..



Jinsi ya kukinga kupoteza hamu ya kula kwa watoto:

·         Fanya vyakula viwe na muonekana wa kuvutia kwa mtoto. Kwa mfano: unaweza kupakua chakula kwenye sahani yenye umbo la kitu anachopenda mtoto, labda sahani yenye umbo la Gari/picha za magari n.k

·         Usibishane na mwanao au kumsema sema inapofika muda wa kula.

·         Rekebisha ratiba ya chakula, umpe mtoto chakula wakati ana njaa.

·         Mtie moyo mtoto kuchagua vyakula vinavyoleta afya.

·         Mruhusu kula kidogo kidogo, kwa nyakati tofauti tofauti.

·         Usimlazimishe mtoto kula kama hana njaa.

·         Usimlazimishe amalize chakula chote kwenye sahani yake, hili sio wazo zuri kwake.

Nyongeza juu ya hapo hizi ni njia za kuongeza hamu ya chakula kwa watoto.
Jinsi ya kuongeza hamu ya chakula kwa watoto.
Hizi ni njia za kuboresha hamu ya kula ya mtoto wako, hizi ni njia za kawaida za nyumbani. Lakini pia nimekuwekea bidhaa bora inayosaidia kwa haraka kuboresha hamu ya kula kuanzia watoto hadi watu wazima.
·         Watoto wanapenda kula vitu vidogo vidogo. Lakini hivi vyakula vidogo vidogo vinapaswa viwe bora kama mlo kabisa. Kwa mfano, mpe mtoto karanga za kukaangwa/korosho badala ya biskuti/crisps.n.k

Karanga zinafahamika kwa uwezo mkubwa wa kuongeza hamu ya kula na kujenga mwili kwa sababu ya kuwa protini. Hata vyakula vyake pendelea kuweka karanga.

·         Mruhusu kucheza/ kujihusisha na mazoezi, hii itamsaidia kupata hamu ya kula vizuri, kuendesha baiskeli, kujihusisha na michezo mbali mbali ni njia bora za kumfanya mtoto awe na hamu ya kula.

·         Kama mtoto amepunguza hamu ya kula mpe chakula kidogo kidogo hadi atakapoanza kula vizuri yeye mwenyewe. Kiasi kidogo cha chakula kitaongeza mmeng`enyo wa chakula na baadae kuongeza hamu ya kula.

·         Mpe chakula chenye kalori nyingi, hii itamsaidia hata akila kidogo tayari atakuwa amepata chakula cha kumsaidia mahitaji ya mwili wake na kuongeza uzito.

·         Mpe maji ya kunywa dakika 30 kabla muda wa kula chakula.

Pia kumbuka….
·         Tumia viungo mbali mbali vya kuongeza ladha ya chakula, hivi vinapatikana kwa urahisi sokoni.
·         Limao, tangawizi, and vinega vinasisimua na kuongeza hamu ya kula.
·         Changanya mboga mboga za rangi tofauti ili ziwe za kuvutia, kwa mtoto wako.
·         Mtengenezee vinywaji vizito (smoothie) kwa kutumia zabibu, asali na maziwa ya mgando.


Kwa maelezo zaidi/maswali na tiba nk.
wasiliana na

Dr. James Makala


jamesmakala40@gamil.com

Phone/ whatsapp 0763832798.


Comments

Post a Comment